Ukimuona mtu amepatwa na degedege, unaweza kuogopa, hasa ikiwa hujui nini cha kufanya. Kwa aina nyingi za degedege, hatua za msingi za huduma ya kwanza ndizo zinazohitajika.
Hatua za kuchukua ni rahisi na mtu yeyote anaweza kuzifanya:

  • kaa na mtu hadi degedege iishe na tazama degedege inadumu kwa muda gani;
  • ondoa vitu vyenye ncha kali karibu yake ili visi mjerui;
  • geuza kichwa cha mtu upande mmoja ili asikose pumzi, weka kitu laini chini ya kichwa chake;
  • usiweke kitu chochote mdomoni kwake kama vile maji, dawa, kibao au chakula mpaka mtu atakapopata fahamu;
  • Usimzuie anapokuwa akitetemeka;
  • kaa pamoja na mtu mpaka hali ya degedege itakapoisha;
  • mpeleke mtu hospitali ikiwa: 
    • degedege imedumu zaidi ya dakika tano;
    • degedege imejirudia mara kwa mara ndani ya siku moja;
    • alipata kifafa majini (bahari/mto);
    • ikiwa amepata majeraha au mjamzito;
    • ikiwa mtu harejei kwenye hali yake ya kawaida;
    • ikiwa ni mara ya kwanza kupatwa na hali hiyo.