Tunatoa huduma kupitia Vituo mbalimbali vya afya vilivyobobea kwenye magonjwa ya kifafa.

Tumezindua Kliniki ya kifafa Ifakara mkoani Morogoro katika Hospitali ya rufaa ya Mt. Francisco pamoja na Hospitali ya INUKA ya utengamao, ilioko Wanging'ombe mkoani Njombe.

Kufikia mwezi Agosti tutatoa huduma hizo Jijini Mbeya katika kituo cha Afya cha Iyunga RC.

Kliniki zetu zina madaktari waliofuzu mafunzo ya kutibu kifafa, lakini pia tunatoa huduma ya kufanya kipimo cha EEG kupitia mashine maalum ambayo hutusaidia kutambua vyema aina ya kifafa ili kutibu kwa dawa sahihi. Hili ni muhimu sana kwa sababu kuna aina tofauti za kifafa na mara nyingi Wahudumu wa afya au wauguzi wa kituo cha Afya/Zahanati hutibu aina zote sawa kutokana na kukosa maarifa na uchunguzi sahihi.