Kifafa kinatibika kwa dawa au wakati mwingine kwa upasuaji.

Dawa zinaweza kusaidia kudhibiti degdege na kupunguza idadi za kutokewa na degedege.

Baadhi ya watu hutibiwa kwa kipindi chote cha maisha yao ili kudhibiti degedege, lakini kuna baadhi degedege huisha kabisa na kifafa kupona. Baadhi ya watoto wenye kifafa, hupona kadri wanavyokua kiumri.

Mara nyingi watu wanakwenda kwenye vituo vya afya au zahanati zenye madaktari wasio na mafunzo ya kutibu kifafa na kupewa dawa zisizo sahihi, ambazo hazimsaidii mgonjwa inayopelekea familia na jamii kudhani kwamba kifafa hakitibiki kwa dawa za hospitalini. Ukweli ni kwamba kifafa kinatibika!

Kama unataka kujaribu huduma zetu, utakutana na madaktari wenye mafunzo na mashine maalum ya kutambua aina ya kifafa na utatibiwa kwa njia bora zaidi hatimaye kupunguza matukio ya degedege.